Michezo
GB 64 amuombea Msamaha rasmi Ali Kamwe kwa Sandaland (Video)
GB 64 AMUOMBEA MSAMAHA ALI KAMWE KWA SANDALAND
Shabiki Maarufu wa klabu ya Simba GB 64 Leo akiwa na Mahojiano na Bongo5 ametangaza kuwa amemuombea Msamaha Afisa Habari wa klabu ya Yanga kwa Sandaland juu ya Bilioni 3 anazotakiwa kumlipa Sandaland.
Pia ameongelea suala la Kocha aliyetimka katika klabu ya Yanga Gamondi kuwa Yanga walikosea kumuondosha Kocha huyo na kumchukua Sead Ramovic kama mbadala wake.
Hakuishia hapo amegusia suala ya Mtangazaji wa Wasafi Media @ricardomomo kutaka kumsaidia mchezaji wa Yanga Prince Dube kutokana na kiwango kisichoridhisha anachokionyesha Mshambuliaji Prince Dube.
Kuangalia Video kamili tembelea ukurasa wetu wa YouTube Bongo5
Imeandikwa na kuandaliwa @Johnbosco_mbanga & Abbrah255