Habari

Gyokeres yuko tayari kujiunga na Man Utd

Mshambuliaji wa Sporting na timu ya taifa ya Uswidi Viktor Gyokeres, 27, yuko tayari kuungana tena na kocha wake wa zamani Ruben Amorim katika klabu ya Manchester United. (Sportsport)

Arsenal imewaongeza winga wa Aston Villa Muingereza Morgan Rogers, 22, na mshambuliaji wa Brazil Igor Paixao, 24, anayechezea Feyenoord, kwenye orodha ya wachezaji wanaopania kuwasajili msimu huu. (Times- usajili unahitajika)

Brentford imekataa dau la kwanza lililowasilishwa na Manchester United kumsajili mshambuliaji wa Cameroon Bryan Mbeumo. Tetesi zinasema Klabu hiyo ya Old Trafford ilitoa pauni milioni 45 pamoja na nyongeza ya pauni milioni 10 lakini The Bees wanataka zaidi ya pauni milioni 60 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Independent)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents