Siasa
Mkurugenzi Masasi asimamishwa kazi kwa ubadhirifu wa fedha
Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa amemsimamisha kazi mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Apoo Tindwa kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za kusaidia maendeleo kwa jamii (CSR) kutoka mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara.
Apoo pamoja na watu wengine wanatuhumiwa kwa ubadhirifu wa zaidi ya Sh5.6 bilioni zilizotolewa na mgodi huo kwaajili ya miradi ya maendeleo katika vijiji 11 vinavyozunguka mgodi huo uliopo wilayani Tarime.