HabariMichezo

Infantino ashinda kiti cha Urais FIFA

Gianni Infantino amechaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kwa muda wa miaka minne.

Infantino mwenye umri wa miaka 52, amepita bila ya kupingwa kwenye kongamano lililofanyika Kigali nchini Rwanda leo siku ya Alhamisi.

Mwanasheria huyo ameiongoza FIFA tangu kuondoka kwa utawala wa Joseph Blatter, mnamo mwaka 2016 na bado anayo nafasi ya kuwania tena mwaka 2027.

Nchi kadhaa za Ulaya, zikiwemo Ujerumani, Norway na Uswidi, hazijafurahishwa na urais wake na zimesema hazitamuunga mkono kikamilifu.

Imeandikwa na @fumo255

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents