Jarida la Lonely Planet limetoa maeneo bora zaidi ya utalii mwaka 2022
Huku hali ikirejea taratibu kuwa ya kawaida duniani baada ya janga la Covid, wale ambao wana mapumziko na wana uwezo wa kwenda likizo tayari wameanza kufikiria kuhusu kusafiri.
Mojawapo ya kuchagua ni wapi kwa kwenda ni kuangalia katika orodha ya mapendekezo ya sehemu za kwenda ya Lonely Planet.
Lonely Planet ambalo ni jarida la wasafiri limechapisha taarifa kuhusu mahali bora zaidi pa kwenda kwa mwaka 2022 wiki iliyopita, huku sehemu hizo zikigawanywa kwa misingi ya nchi, miji na kanda.
Muongozo huo umependekeza sana watu watembelee kisiwa cha Cook- Cook Islands, kilichopo katikati ya bahari ya Pacific ambacho hufahamika sana kwa maji yake safi na fukwe ambazo bado hazijaharibiwa.
“Zaidi ya ubora wake wa kiutalii na muonekano wenye mvuto wa kisiwa chenyewe, kina utajiri wa utamaduni, kikiwa na maadili ya utamaduni wa Polynesia”, umeeleza muongozo huo.
Maeneo mengine yaliyoljitokeza kuwa bora ni Oman , eneo muhimu kwa wapenzi wa historia na udadisi. Eneo hili limejaa makasri, ngome na misikiti.
Nchi hii ina utajiri wa kitamaduni na maeneo ya urithi wa dunia, kama vile Ngome ya Bahla na mji wa kale wa Qalhat , pamoja na maeneo mengine yenye uzuri asilia majangwa na mwambao safi ambao haujaharibiwa.
Amerika Kusini
Lonely Planet haikusahau eneo la Amerika Kusini ambapo limetaja mji wa Mexico wa Mérida katika orodha ya miji bora zaidi na jangwa la Chile la Atacama
Merida
Muongozo huo umetaja historia ya ukoloni ya Mérida, mji maarufu zaidi uliopo katika jimbo la Yucatán, unaopatikana Kusini mashariki mwa nchi, na “sifa yake ya mchanganyiko wa maisha ya kimkoa na yasiyofuata utawala wowote .”
“Ni eneo zuri kulitembelea kwa lengo la kujifunza, likiwa na mitaa meembamba medani kubwa za kati, na majumba makubwa ya katika kanda hiyo.”
“Pia ni eneo linalofaa zana kuanzisha safari yako ya uzoefu mpya kuelekea katika jimbo la Yucatan. Lina mapishi bora na malazi, masoko yanayoshamiri, na matukio yanayofanyika kila usiku.”
Atacama
Kuhusiana na jangwa la Atacama , muongozo huo unatoa hakikisho kwamba kuna mandhari ya kuvutia kuwahi kushuhudiwa katika sayari.
Likipatikana kaskazini mwa Chile, jangwa la Atacama lina ukubwa wa kilomita za mraba takriban 105,000 likiwa ndio jangwa kubwa zaidi duniani.
Jangwa hili ambalo liko mbali na uchafuzi wa mazingira wa maeneo ya miji mikubwa ni eneo bora la kuvinjari.
Puerto Rico pia inapatikana katika orodha hii kutokana na uzuri wake wa kipindi cha ukoloni kilichopita na ule wa asili.
Hii hapa ni orodha nzima kulingana na muongozo wa jarida la Lonely Planet:
1.Nchi
•Kisiwa cha Cook
•Norway
•Mauricio
•Belize
•Slovenia
•Eel
•Oman
•Nepal
•Malawi
•Misri
2. Cities
•Auckland, New Zealand
•Taipei, Taiwan
•Freiburg, Ujerumani
•Atlanta, Marekani
•Lagos, Nigeria
•Nicosia, Cyprus
•Dublin, Ireland
•Merida, Mexico
PICHA: Hidalgo Park, Merida, Mexico.
•Florence, Italia
•Gyeongju, Korea Kusini
3. Kanda
•Westfjords, Iceland
PICHA: Westfjords, Iceland
•West Virginia, Marekani
•Xishuangbanna, China
•The Kent coast, Uingereza
•Puerto Rico, Marekani
•Shikoku, Japan
•Jangwa la Atacama, Chile
•Scenic Rim, Australia
•Kisiwa cha Vancouver, Canada
•Burgundy, Ufaransa