Jean Baleke anafikisha idadi ya magoli 7 na kama angekuwa amesajiliwa tangu mwanzo wa msimu basi Fiston Mayele tungezungumza mengine.
Baleke ana muda mchache tu ndani ya Ligi Kuu lakini tayari anawakaribia vinara wa magoli.
Yanga alikufa kwenye dimba hili la Highland Estate, Azam FC, KMC, Mtibwa Sugar, Mbeya City wote wamekufa kwa Ihefu kwenye uwanja huo lakini Jean Baleke ameutafuna mfupa uliyowashinda miamba hiyo.
Imeandikwa na @fumo255