HabariSiasa

Jeshi la Israel limekusanyika mpakani mwa Gaza kabla ya mashambulizi

Jeshi la Israel linasema linapanga mashambulizi ya ardhini, angani na baharini – lakini hatujui ni lini mashambulizi ya ardhini yanayotarajiwa yataanza.

Jumamosi jioni, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alitembelea wanajeshi waliokuwa wakijiandaa kwa shambulizi hilo.

Picha za video zilimuonyesha akiwa amevalia fulana ya kuzuia risasi akiongea na wanajeshi waliokuwa na silaha nzito katika makazi ambayo yalikuwa yakilengwa na wanamgambo wa Hamas katika shambulio la Jumamosi iliyopita, walipojipenyeza Israel.

“Uko tayari kwa kile kinachokuja? Mengi zaidi yanakuja,” anasema kwenye video.

Mashambulizi makali ya anga ya Israel yaliendelea usiku kucha. Mamilioni ya watu wa Gaza wametakiwa kuhama kaskazini mwa eneo hilo – huku wengi wakitoroka kwa gari au kwa miguu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents