Habari
Jubilee Insurance sasa kuwaangalia chama cha waendesha Baiskeli Tanzania
No CHAMA CHA WAENDESHA BAISKELI TANZANIA SASA NI ZAMU YAO LIVE FREE RACE
Siku ya leo Taasisi ya @jubileeinsurancetanzania imetangaza rasmi kuwashirikisha Chama cha waendesha Baiskeli Tanzania kwa kuwapeleka wanamichezo wa mchezo huo nchini Kenya kwenye mashindano ya Live free race ili kwenda kupeperusha bendera ya Tanzania nchini Kenya katika jiji la Nairobi.

Mashindando hayo yanatarajiwa kuanza mnamo tarehe 5/10/2025 huku Mataifa mbalimbali yakihusika katika mashindano hayo.
Timu ya Tanzania ya Waendesha Baiskeli tayari imeshawasili nchini Kenya katika jiji la Nairobi na wanamichezo wanne watakaoipeperusha Bendera ya Tanzania katika mashindano hayo nchini Kenya.




