Burudani
Kanye West awashawishi mashabiki wake wazisuzie bidhaa za brand ya Louis Vuitton
Kanye West amewataka mashabiki wake wazisusie bidhaa mbalimbali (mikoba, mabegi, nguo, saa na vingine) za brand ya Louis Vuitton.
Rapper huyo alipiga stunt hiyo wakati wa mahojiano na kituo cha radio ambako alielezea hasira yake baada ya kutoshwa na makamu rais wa brand hiyo, Yves Carcelle. Akiongea na 92.3 NOW radio, Kanye alisema: ‘Nilitengenezwa kwa wasaa huu. Kilichotokea ni kwamba wakati nikiwa Paris nilitaka kukutana na mkuu wa Louis Vuitton, alisema ‘sielewi kwanini tunahitaji kuonana na wewe’.’Nilisema, “acha nieleze kwanini unahitaji kuonana na mimi. Kila mtu jijini New York kwa sasa hanunui Louis Vuitton yoyote hadi baada ya January. Sasa unataka kukutana name? Ushawishi. Hawajui kuwa sitambui nguvu.’