Habari
Kanye West kugombea Urais Marekani mwezi Novemba 2020
Kanye West kugombea Urais Marekani mwezi Novemba 2020
Msanii wa muziki wa Hip Hop kutoka Marekani Kanye Omari West maarufu kama Kanye West ametangaza nia yake ya kuingia katika kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha Urais wa taifa hilo tajiri duniani.
Kanye West akimuonyesha picha Rais wa Marekani Donald Trump ilipokutana naye katika Ikulu ya White House mwaka 2018
Kanye West ameonyesha nia hiyo ya kugombea Urais wa Marekani katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 3 Novemba siku ya Jumanne mwaka huu 2020.
Yeezy, amesema sasa lazima watambue ahadi na ndoto za Wamarekani zitatimia kwa kumuanini Mungu, kuunganisha maono yao pamoja na kuijenga kesho iliyo bora.
Imeandikwa na Hamza Fumo