Afya

Kenya yaanza kuwadunga watu chanjo ya Corona (+ Video)

Kenya imeanza kutoa chanjo ya Corona leo na mtu wa kwanza ambaye amedungwa chanjo hiyo ni kaimu mkurugenzi wa afya Patrick Amoth.

Watu kumi wa kwanza pia wamedungwa chanjo hiyo katika hospitali ya Kenyatta jijini Nairobi .

Wengine waliochanjwa ni afisa mkuu mtendaji wa hospitali ya Kenyatta Evanson Kamuri akifuatwa na muuguzi mmoja wa hospitali hiyo kisha Collins Tabu ambaye ni mkuu wa kitengo cha Chanjo katika wizara ya afya akachanjwa pia.

Wote walioachanjwa walitakiwa kusaini mkataba wa kuidhinisha kupewa chanjo hiyo na baadaye wakatakiwa kupumzika kwa dakika 30 kabla ya kuruhusiwa kuondoka .

Katibu wa kudumu wa wizara ya Afya Susan Mochache amesema chanjo itatolewa katika hospitali zote za rufaa za kaunti pindi uzinduzi katika hospitali ya KNH utakapokamilishwa .

Mwakilishi wa WHO nchini Kenya Rudi Eggers amesema Wakenya hawatagharamika wanapodungwa chanjo hiyo ya AstraZeneca.

Bofya hapa chini kutazama.

https://www.instagram.com/tv/CMEu4GlB5M8/

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents