Michezo
Kesi ya Sabaya yaendelea kusikilizwa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha leo inaendelea na usikilizwaji wa shahidi namba mbili wa kesi ya Jinai namba 105 ya mwaka 2021 ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili.
Usikilizwaji wa shahidi huyo namba mbili Numan Jasini (17) unaendelea baada ya kuahirishwa kupisha mapumziko ya sikukuu ya Eid Al Adha.