Michezo
Kesi ya Yanga na Morrison imekwisha CAS, fahamu zaidi
Mahakama ya kimataifa ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) leo imemaliza kulisikiliza kesi ya rufaa ya Klabu ya Yanga dhidi ya Bernard Morrison. Mara baada ya kumalizika kusikilizwa kwa kesi hiyo, CAS itatoa uamuzi kwa mujibu wa taratibu zake kuanzia sasa mpaka tarehe 14/08/2021.