Habari

Kimbunga ‘Ian’ chaipiga Cuba, wasiwasi waibuka Florida

Kimbunga kilichopewa jina la Ian Jumaane kiligonga magharibi mwa Cuba kwa kishindo, na kuwaacha takriban watu milioni 1 bila umeme, kisha kikachukua mkondo unaoonekana kulenga pwani ya Florida huku kikitarajiwa kuongezeka nguvu na kuwa dhoruba ya kiwango cha 4.

Ian kiligonga mkoa wa Pinar del Rio nchini Cuba, ambapo serikali iljenga makazi 55 ya muda kuwahamisha watu 50,000, kuwapeleka wafanyakazi wa dharura kwenye maeneo yaliyoathiriwa, na kuchukua hatua za kulinda mazao katika eneo linalokuza tumbaku nyingi zaidi nchini humo.

Kituo cha Kitaifa cha Vimbunga cha Marekani kilisema Cuba iliathiriwa pakubwa na upepo na dhoruba wakati kimbunga hicho kilipopiga, kikiwa na upepo wa kasi ya kilomita 205 kwa saa.

Kimbunga Ian kilitarajiwa kupata nguvu zaidi katika Ghuba ya Mexico, na kufikia kasi ya zaida ya kilomita 209 kwa saa, kinapokaribia pwani ya kusini magharibi mwa Florida, ambako watu milioni 2.5 waliamriwa kuhama makazi yao.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents