FahamuHabari

Kocha wa makipa wa klabu ya Simba akamatwa kwa madawa ya kulevya

Mammlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imewakamata watuhumiwa 11 akiwemo kocha wa makipa wa timu ya Simba Club, Muharami Sultan (40) anayetuhumiwa kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin na bangi.

Hayo yameelezwa leo Novemba 15 na Kamishna Jenerali wa DCEA, Gerald Kusaya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mbali na Muharami Sultani anayedaiwa kukutwa na kilo 34.89 za dawa za kulevya aina ya heroin na biskuti 50 zilizotengenezwa kwa kutumia dawa ya kulevya aina ya bangi, wengine waliotajwa ni pamoja na mmiliki wa kituo cha Cambiasso Sport Academy kilichopo Tuangoma, Kambi Zuberi seif, Said Matwiko mkazi Magole.

Wengine ni Maulid Mzungu maarufu mbonde (54) mkazi wa kisemvule na John John maarufu Chipanda (40) ambaye jukumu lake kutafuta vijana wenye vipaji na kuwapeleka Cambiasso Sport Academy.

Wengine ni Rajabu Dhahabu (32) mkazi wa Tabata, Seleman Matola Said (24) mkazi wa Temeke Wailes, Hussein Pazi (24) na Ramadhani Chalamila (27).

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents