Burudani

Kuongea Kiingereza ni kipaji – Shilole

Msanii wa muziki, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kwa kudai kuongea Kiingereza siyo kitu cha mchezo kama watu wanavyofikiria.

Shilole-2

Akizungumza katika kipindi cha Enewz cha East Africa Television Jumatano hii, Shilole alisema yeye amepigana mpaka ameweza kuongea Kiingereza.

“Kiingereza ni kipaji jamani, mimi naongea Kiingereza wakati ambao najisikia. Lakini asikwambie mtu, kuongea Kiingereza ni kipaji,” alisema Shilole.

Muimbaji huyo ameachia kazi mpya iitwayo ‘Say My Name.’

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents