Michezo

Kurt Zouma akiri makosa ya kumpiga paka

Nyota wa mpira wa miguu wa West Ham, Kurt Zouma amekiri mashtaka yake mahakamani alimpiga teke na kibao paka wake mwezi Februari mwaka huu.

Februari mwaka huu ilisambaa video ya Zouma akimpiga paka, video hiyo iliwekwa katika mitandao ya kijamii na mdogo wake Yoan.

Zouma amekiri alitenda makosa kwa kuvunja sheria ya ustawi wa wanyama. Kesi yake itasikilizwa tena Juni 1 mwaka huu. Paka wake alichukuliwa na Jumuiya ya Kifalme ya Kuzuia Ukatili (RSPCA) na anatafutiwa makazi mapya.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents