HabariMichezo

LeBron James ndio mfungaji wa muda wote NBA

LeBron James amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa NBA, akipita rekodi ya Kareem Abdul-Jabbar ya miaka 39.

Nyota huyo wa Los Angeles Lakers James, 38, alifikisha pointi 38 katika kushindwa 133-130 na Oklahoma City Thunder na kuvuka alama ya Abdul-Jabbar ya 38,387.

Awali Abdul-Jabbar alivunja rekodi ya kufunga mabao Aprili 1984, miezi minane kabla ya James kuzaliwa.

“Kuweza kuwa mbele ya gwiji na mtu stadi kama Kareem, ina maana kubwa kwangu,” alisema James.

James mwenye hisia aliinua mikono yote miwili kusherehekea huku Abdul-Jabbar mwenye umri wa miaka 75, ambaye alikuwa kwenye mechi katika uwanja wa nyumbani wa Lakers, alisimama na kupiga makofi.

Kulikuwa na mapumziko mafupi kwa ajili ya sherehe ya kuashiria mafanikio, huku James akichukua kipaza sauti ili kutoa hotuba fupi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents