Makali ya Chikwende nafasi za Kahata, Ajib zitabaki salama ?, uchambuzi na Abbas Pira (+Video)
Mabingwa watetezi Ligi Kuu Tanzania Bara Simba SC mapema mwishoni mwa wiki hii wame mtambulisha rasmi kiungo wao mpya raia wa Zimbabwe Perfect Tatenda Chikwende aliyejizoelea umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijamii hasa baada ya mchezo wao wa kwanza wa FC Platinum dhidi ya Simba SC. Uwezo mkubwa aliyo uonyesha Chikwende katika michuano ya CAF Champions League, akishuka uwanjani mara nne (4) na kufunga magoli mawili (2) pengine ni moja ya sababu ya Wekundu wa Msimbazi kumvuta karibu nyota huyo. Je, uwepo wake ndani ya kikosi cha Mnyama Simba, nafasi za Kahata, Ajibu, Morrison na baadhi ya wachezaji wengine wanaocheza nafasi hiyo ya kiungo cha ushambuliaji watabaki salama ?. Abbas Pira anaangazia uwezo wa Mzimbabwe huyo mwenye umri wa miaka 27.