Michezo

Manchester United waingia sokoni

Kunako tetesi za soka huko barani Ulaya, miamba ya soka pale Hispania klabu ya Barcelona wanafikiria uhamisho wa mshambuliaji wa Manchester City na timu ya taifa ya England, Raheem Sterling mwenye umri wa miaka 26. (Mundo Deportivo – in Spanish)

Lakini pia Barcelona wapo kwenye mazungumzo na kiungo wa kati wa zamani wa Uhispania Xavi, 41, kuhusu kuchukua nafasi ya kocha Ronald Koeman. (90min)

Pale kwa Malkia, Uingereza miamba ya soka Manchester United inafikiria kumpata kiungo wa kati wa AC Milan Franck Kessie,24, kama mbadala wa Paul Pogba. (Calcio Mercato – in Italian)

Manchester City kwa upande wao wanamfuatilia kwa karibu mno kiungo wa kati wa Uhispania Nico Gonzalez anayekipiga Barcelona (Fichajes – in Spanish)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents