Mara ya sita Vilabu vya England kukutana Ulaya

- Chelsea 1-0 Man City (UCL, 2021)
- Spurs 0-2 Liverpool (UCL, 2019)
- Chelsea 4-1 Arsenal (UEL, 2019)
- Man United 1-1 Chelsea (UCL 2008, Man U alishinda 6-5 kwa penati)
- Spurs 3-2 Wolves (UEFA Cup, 1972 – fainali ya mikondo miwili)
Tofauti na fainali zilizopita, mechi ya Spurs vs United inakutanisha vilabu vilivyokuwa dhaifu msimu mzima lakini vinapigania kutengeneza heshima Ulaya.
Manchester United na Spurs wamekuwa na kampeni za ligi mbaya kihistoria. Kwa msimu wa 2024-25 tayari umethibitisha Man Utd atamaliza na alama za chini kabisa katika msimu wa ligi tangu mwaka 1973-74, na endapo watashindwa kuifunga Aston Villa katika mechi ya mwisho ya msimu, itakuwa rekodi yao mbaya zaidi tangu msimu wa 1930-31 (walipopata alama 29).
Spurs wao wana alama 38 tu katika mechi 37 za ligi msimu wa 2024-25, na iwapo watapteza mechi yao ya mwisho ya msimu dhidi ya Brighton, itakuwa kampeni yao ya pili mbaya zaidi ya ligi katika historia baada ya ile ya 1914-15 (alama 36). Sasa wamepoteza mechi 25 katika mashindano yote msimu huu, idadi yao kubwa zaidi ya vipigo katika msimu mmoja katika historia yao ikilingana na ile ya msimu wa 1991-92 ilipopogea vipigo 25).
Kuelekea siku ya mwisho ya kampeni ya Ligi kuu mwishoni mwa wiki hii, United na Spurs wako mkiani katika msimamo, United ya 16 na Spurs ya 17, nafasi za chini kabisa baada ya zile tatu zilizoshuka daraja.
Sasa fainali ya leo ni tofauti kidogo: si vita ya kifahari, bali ni sawa na pambano la mwisho la vilabu vilivyokata tamaa. Kwa Spurs, ni nafasi ya kuandika upya historia ya Ulaya baada miaka 41. Kwa United, ni tumaini la pekee la kubeba taji la kwanza chini ya Ruben Amorim.
Kwa hiyo katika mji wa kihistoria wa Bilbao huko Hispania, leo usiku si tu hatima ya kombe inayotazamwa, bali historia mpya ya klabu moja wapo itazaliwa. Kati ya Tottenham na Manchester United, ni nani ataibuka shujaa wa ukombozi?