HabariMichezo

Marekani yaitaka Urusi ikubali dili ya kumuachilia nyota wa vikapu aliyefungwa jela miaka 9

Marekani imeitaka Moscow kukubali makubaliano ya kumwachilia mchezaji wa mpira wa vikapu Brittney Griner, ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka tisa jela nchini Urusi.

Mshindi huyo mara mbili wa Olimpiki alipatikana na hatia ya kumiliki na kusafirisha dawa za kulevya baada ya kukiri kuwa na mafuta ya bangi.

Msemaji wa usalama wa taifa wa White House John Kirby alisema pendekezo la Marekani ni “pendekezo zito”, lakini hakutoa maelezo zaidi.

Ripoti za vyombo vya habari vya Marekani zinaonyesha kuwa Washington inapeana ubadilishaji wa wafungwa unaohusisha mlanguzi wa silaha wa Urusi.

Viktor Bout – anayejulikana kama “mfanyabiashara wa kifo” – anatumikia kifungo cha miaka 25 jela nchini Marekani.

Anaweza kuhamishwa na Washington kwa mamlaka ya Urusi badala ya Griner na mwanajeshi wa zamani wa Marekani Paul Whelan, ripoti zinasema.

Whelan, ambaye ana hati za kusafiria za Marekani, Uingereza, Kanada na Ireland, alihukumiwa mwaka 2020 hadi miaka 16 jela nchini Urusi baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ujasusi.

Bw Kirby aliwaambia wanahabari kwamba wawili hao walikuwa wakizuiliwa kimakosa na walihitaji kuachiliwa huru .

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents