Msanii wa muziki wa Bongo Fleva @mauasama amekuja kivingine kwenye suala la Listening Session baada ya kuzindua ATM maalumu kwa ajili ya kusikiliza muziki.
Maua Sama amekuja na wazo hilo ambapo amewapa nafasi mashabiki ya kusikiliza na kuangalia video mpya ya ngoma yake kwa wakati mmoja.
Akiongea na Waandishi wa Habari meneja wa @mauasama Micharl amefafanua namna ambavyo waliandaa utaratibu wa kuwapa nafasi Mashabiki ya kusikiliza wimbo na kuangalia video kwa wakati mmoja.