Beki wa Coastal Union raia wa DR Congo, Pascal Kitenge amemtumia ujumbe Mshambuliaji wa Klabu ya Wananchi, Fiston Mayele kuelekea fainali ya Azam Sports Federation Cup kati ya Yanga SC dhidi ya Coastal Union ambayo itapigwa dimbani Sheikh Amri Abeid, Arusha Julai 2, 2022.
Kitenge amemwambia Mayele kuwa watakutana tena Arusha na hataifunga tena Coastal Union FC kama alivyofanya hivyo kwenye michezo iliyopita.
“Fiston tukutane Arusha, unatufunga Tanga unatufunga Dar es Salaam, Arusha hautufungi,” maneno ya beki wa Coastal Union, Pascal Kitenge
Fainali hiyo ya Azam Sports Federation Cup kati ya Yanga SC dhidi ya Coastal Union itapigwa kwenye dimbani la Sheikh Amri Abeid, Arusha Julai 2, 2022.
Imeandikwa na Hmaza Fumo, Instagram @fumo255