FahamuHabari

Mazingira ya Utalii Dubai yazidi kuboreshwa

Tarehe 2,disemba 2022 ilikua ni siku rasmi ambayo umoja wa falme za kiarabu wamesherehekea siku ya taifa kwa mara ya 51 na wanaalika watu wote duniani kushiriki katika sherehe hizo mpaka leo hii.
Dubai kumekua na matamasha mbali mbali, fataki,michongo ya kufanya shopping kwa bei rahisi zaidi, yote yakiandaliwa na Dubai Festival and Retails Establishment (DFRE)

Sherehe hizi zimeanza rasmi siku ya tarehe 2 disemba na zinaendelea mpaka tarehe 9 disemba ambapo ni siku 10 za sherehe hizo bila kusimama.

Ahmed Al Khaja (CEO wa DFRE) amesema siku hizo ni za sherehe za kusherehekea ukuaji wa falme za kiarabu, uvumbuzi ambao umekua ukiendelea kwa asilimia kubwa na kuungwa mkono na sekta ya reja reja (Retail sector) ambapo urithi wa nchi hiyo utaendelezwa kwa kulileta taifa pamoja na kusherehekea.
Hivi sasa Dubai kumependezeshwa na mapambo kila eneo la mji huo, fataki zenye ramani za nchi hiyo zinazoonekana sana maeneo kama Al seef, Dubai Festival city mall n.k
Matamasha maeneo ya Al wasl plaza (Expo city), Dubai Opera na maeneo mengine mengi.
Migahawa mingi pia imeleta ofa za kula vyakula kwa bei rahisi zaidi katika kipindi hiki bila kusahau utazamaji wa live wa mashabiki pale Dubai Harbour kwenye Bud X Fifa fan festival.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents