Michezo

Mbinu gani Simba watumie kuwadhibiti Al Ahly ndani ya dakika 90, Abbas Pira achambua (+Video)

Kuelekea kwenye mchezo Mkubwa na wenye kuangaziwa na watu wengi wapenda soka Barani Afrika na pengine duniani kwa ujumla baina ya Mnyama #simbasc ya Tanzania dhidi ya Mafarao wa Misri klabu ya Al Ahly Jumane ya wiki ijayo. Kumekuwa na maoni mbalimbali kwa wadau hao wa kabumbu kuwa ni kitu gani wanaume 11 wa Simba watapaswa kufanya pale kwa Mkapa ndani ya dakika 90 ili tu kuhakikisha wanabakiza alama tatu nyumbani.

Licha ya Simba kuonekana bora lakini wanakutana waliyobora zaidi ambao ni Al Ahly, @abbas__pira ametoa mtazamo wake kile ambacho vijana hao watapaswa kukifanya na kukitimiza uwanjani kwa asilimia 100.

Sio mara ya kwanza Simba kuibuka na ushindi nyumbani dhidi ya Al Ahly kwenye michuano Afrika, lakini Al Ahly hii inaonekana kuwa Yamoto, kabla ya kutua Dar, wametoka kumkabili Bingwa wa UEFA Champions League Bayern Munich, lakini wakampiga El Merreikh nyumani huku usisahau kuwa hawa ndiyo Mabingwa mara nyingi zaidi wa Michuano hii ya Klabu Bingwa Afrika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents