Mbunge wa Jimbo la Ukonga DaresSalaam Jerry Silaa, ametoa malalamiko yake kwa Mamlaka zinazohusika na ujenzi wa miundombinu ikiwemo #TANROADS kwa kupuuzia maagizo ya viongozi katika utoaji wa kandarasi za ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo barabara za mwendokasi jijini Dar es Salaam.
Katika kuonyesha kutoridhishwa Mbunge huyo ameshindwa kuzuia hisia zake za machozi huku akisisitiza kuwa wakandarasi wanaoshindwa kutekeleza kazi kwa viwango wasipewe kandarasi nyingine kwa kuwa hali hiyo inakihatarisha chama na wabunge wao pindi inapofika wakati wa uchaguzi.