BurudaniHabari

Meja Kunta ashikwa na kiwewe baada ya kuitwa BASATA, naombeni msamaha

Kupitia Instagram yake staa huyo wa Singeli nchini ameandika kuwa:

“Nimepata barua ya wito kutoka kwa wasimamizi na walezi wa Sanaa yetu @basata.tanzania ikinitaka kuhudhuria siku ya Kesho na ni kutokana na CHALLENGE ya wimbo wangu mpya wa SHUU ambao nimemshirikisha #BABALEVO & #NTOSHGANZ kutoka Afrika ya kusini maana nilikuwa napambania ndoto yangu ya kuipeleka Singeli kimataifa.

Ni Mara ya kwanza kwangu, kuitwa na @basata.Tanzania hivyo napata mawazo mengi sana, Ninaomba kesho nisindikizwe na Kaka yangu #babalevo Japo ningependa na #ntoshi awepo sema umbali utamzuia.

Mziki ni Marsha yetu, tumetoka hali Duni sana na familia zetu zinapata unafuu kwa kupitia vipaji vyetu, walezi wangu @basata.Tanzania Kijana wenu nitakuja kama barua ilivyonitaka natumai tutakuwa na mazungumzo yakujenga na mwisho NINAOMBA RADHI KWA YEYOTE aliyepata shida/kuudhiwa na challenge ile, naomba mniwie radhi sana KIJANA WENU BADO NAJITAFUTA

Kama hujatazama na kusikiliza audio hii, link hiyo hapo chini

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents