Wakati Dunia itasimama kwa muda kupisha mbungi ya fainali ya Kombe la Dunia pale Qatar baina ya Argentina dhidi ya Ufaransa.
Mwamuzi wa kati atakaye simamia sheria 17 za mchezo wa kabumbu hii leo Jumapili ya Desemba 18, 2022 ni Szymon Marciniak.
Szymon Marciniak amesema sababu kubwa iliyopelekea yeye kuwa mwamuzi wa soka ni baada ya kupewa kadi nyekundu na kutolea nje kutokana na kumtusi mwamuzi akiwa anacheza uwanjani.
Mwamuzi huyo mwenye umri wa miaka 41 amekumbuka tukio hilo la ujanani mwake akiwa mchezaji tegemezi baada ya kuchezewa faulo na kumlalamikia mwamuzi ampe kadi nyekundu mpinzani wake.