Burudani

Mimi na mume wangu tutafunga ndoa ya kawaida kabisa – Lulu

Msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael (Lulu) ameelezea juu ya tetesi za yeye kufunga ndoa kimya kimya na mpenzi wake Francis Siza (Majizzo).

Akizungumzia na Clouds FM, Lulu amesema kuwa habari hizo hazina ukweli na harusi yao itakuwa ya kawaida kama watu wengine, akisisitiza kuwa hakutokuwa na haja ya kuficha wala kufunga kwa siri.

Mimi na mume wangu mtarajiwa tutafunga ndoa ya kawaida kabisa kama zilivyo harusi nyingine, tutakuwa na familia pamoja na ndugu na jamaa“, amesema Lulu.

Mwanadada Lulu mwishoni mwa mwaka jana alivishwa pete ya uchumba na siku kadhaa baadaye alitolewa mahari na mchumba wake huyo na kinachosubiriwa hivi sasa ni harusi yao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents