Afya

Misri kama hujachanja, hutaruhusiwa kwenda kazini

Misri itawazuia wafanyikazi wa umma ambao hawajachanjwa dhidi ya kuingia katika majengo ya serikali kutoka katikati ya mwezi ujao.

Ilani ya baraza la mawaziri Jumapili ilisema wafanyikazi watalazimika kupewa chanjo au kufanyiwa vipimo vya Covid kila wiki ili waruhusiwe kuingia kwenye majengo ya serikali kutoka 15 Novemba.

Baraza la mawaziri pia liliruhusu kufunguliwa kwa bafu katika misikiti kutoka Jumatano.

Bafu zilifungwa mnamo Machi mwaka jana kama sehemu ya hatua za kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona Serikali pia imetenga pauni bilioni Moja za Misri ($ 64m; £ 47m) kushughulikia janga hilo.

Misri imetoa chanjo zaidi ya milioni 30 kwa raia wake dhidi ya idadi ya watu zaidi ya milioni 100, kulingana na data kutoka kwa wizara yake ya afya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents