Habari

MNEC Dar Majid Nassor alivyompandisha jukwanii Luca Mgombea Udiwani Kata ya Msasani (Video)

MNEC CCM Mkoa wa Dar Es Salaam Ndg. Yusuph Majid Nassor amefunguka kuzunguzia uwezo wa mgombea Udiwani Kata ya Msasani Luca Neghesti katika mkutano wa Diwani huyo uliofanyika Namanga Jijini Dar Es Salaam.

“Nimewaletea diwani wa Kata ya Msasani ndugu Luca, hakuna mwingine atakuja kuwaletea maendeleo zaidi ya Diwani ambaye tuko naye hapa mbele. Tunawaletea diwani ambaye anayejielewa, anayejitambua na mwenye elimu yake, lakini sio diwani anayekwenda Manispaa kupiga ‘blabla’ anakwenda kufanya kazi ili kuleta maendeleo kata ya Msasani,” alisema Majid.

Aliongeza, “Na msiogope rangi yake, huyo sio mzungu anapiga kiswahili kama Mndengereko, tumeleta diwani Mndengereko mwenzetu,”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents