Burudani

Msimamo wa WCB, ‘Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu’ (+video)

Label ya WCB imezungumza kuhusu baadhi ya vyombo vya habari kutopiga nyimbo za wasanii wao.

Miongoni mwa mameneja wa WCB, Babu Tale leo katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam amesema kwa vile vyombo hivyo viliwakataa mwanzo na sasa waendelee hivyo hivyo.

‘Tunaendelea kuwaomba waendelee kushinikiza wafanyakazi wao wasipige nyimbo zetu,” amesema.

“Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu kwa sababu wao walitukataa mwanzo, tunawakataa kwa sababu wao walitukataa,” amesema Babu Tale kwa msisitizo.

Hapo awali Diamond Platnumz alisema siku zote katika tasnia mbali mbali michezo ya kubaniana ipo ila hawezi kulaumu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents