Michezo
Mtukutu ‘Super’ Mario Balotelli kurejea England
Newcastle imehusishwa kutaka kumrejesha England mtukutu ‘super’ Mario Balotelli katika dirisha la usajili. Balotelli ambaye kwa sasa anaitumikia Adana Demirspor ya nchini Uturuki, lakini kwa sasa anaangaziwa kama moja ya sajili itakayozungumzwa zaidi.
Klabu ya Barcelona imehusishwa kutaka kuwasajili, Timo Werner, Pierre-Emerick Aubameyang na Edinson Cavani. Kwa mujibu wa Mundo Deportivo wachezaji hao wanaweza kusajili dirisha hili la mwezi Januari ama hata lijalo.
Watford imeridhia dili la paundi milioni 3.5 kutoka Bordeaux FC ya Ligue 1 dhidi ya winga Mnigeria, Samuel Kalu (24).