Muziki
MUSIC AUDIO: Vichou Ft. Magic Washington – Who Can Love Me
Msanii wa muziki maarufu kutoka Bujumbura nchini Burundi, Vichou ameachia kazi yake mpya ya ngoma ya ‘Who Can Love Me’ akiwa amemshirikisha msanii mwenzake kutoka Uganda, Magic Washington.
Uzuri ni kwamba, Video ya ngoma hii tayari imesharekodiwa nchini Uganda na inatarajia kuachiwa muda si mrefu.
Bongo5 imepiga stori na Meneja wa Vichou, Happy Famba kutoka Burundi amesema kuwa “kila kitu kipo tayari na kinachosubiriwa ni muda tu kuachia video ya ” Nani atakayenipenda” Na msanii wangu alitafutwa na Magic na nikaona ni muda muafaka kufanya kolabo. Kuhusu wasanii wa Tanzania nawakubali na msanii wangu atafanya kolabo nyingine baada ya Lady JayDee”
Bofya link hapo chini kusikiliza ngoma mpya ya Vichou na kisha udondoshe komenti yako..