Staa wa muziki wa Bongo Fleva @officialnandy tayari ametoa orodha ya ngoma zinazopatikana kwenye EP yake mpya ya MATURITY.
EP hiyo yenye ngoma tano ameshirikisha wasanii tofauti tofauti akiwemo msanii mchanga wa Bongo Fleva #Lody Music.
Mbali na Lody Music wasanii wengine ni Dulla Makabila kutoka Tanzania ambaye ypo kwenye track namba 4, Oxlande kutoka nchini Nigeria ambaye yupo kwenye wimbo namba 1 lakini pia Nviiri the storyteller kutoka Kenya kwenye wimbo namba 2 lakini kwenye wimbo wa mwisho ni msanii Natty kut0ka nchini Marekani kwenye wimbo namba 5.