Bongo5 Exclusives
Ngumi: Mfaume Mfaume atema cheche baada ya kumtwanga Keisi Ally ”Yoyote atakayekuja nampiga kwa KO” (+Video)
Bondia Mfaume Mfaume amesema kuwa kwa sasa yoyote atakayekuja kupambananaye basi atahakikisha anampiga kwa KO, mwanamasumbwi huyo ameyasema hayo baada ya kutoka kumchapa mpinzani wake, Keisi Ally kwa TKO.
Mfaume Mfaume amezipiga na Keisi Ally kwenye mchezo wa ufunguzi kabla ya pambano kuu baina ya Mtanzania Hassan Mwinyo na Mfilipino, Arnel Tinampay hawajapanda ulingoni.