Habari

Niliwaona malaika wakimbeba TB Joshua – Nabii Paul

Katika video iliyosambaa sana, mjumbe wa Mungu Nabii Paul alitabiri kwamba aliwaona malaika, waliomchukua nabii TB Joshua kutoka duniani.

“Mungu alinionesha maono ya mwisho, nisikieni, nilisimama, na nikachukuliwa juu mbinguni, na madirisha ya mbingu yakafunguliwa kwa ajili yangu, na nikasimama kuangalia chini duniani .”

Niliwaona malaika sita walitumwa chini kutoka mbinguni na kwenda duniani kumbeba nabii Joshua, kile nilichokiona nilikisema.

Malaika watatu walimshika mkono wake wa kuume watatu wakamshika mkono wake wa kushoto, wakambeba juu nabii TB Joshua na kushikilia kikombe.

Nabii Paul alisema alitazama mahala ambapo manabii walisimama, na wakageuka kulia , pia aliweza kuangaliakulia lakini hakuweza kuona sura ya aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha enzi.

Nabii ME Paul pia alisikia sauti ya Mungu akiwaambia malaika kuchukua kikombe cha ndege kutoka kwa Nabii Joshua, na kukileta kwake.

Kwa namna hiyo, nabii alipelekwa mahali sahihi.

“Wakati mmoja hata niliwaona malaika wakuu wakiwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, na wakachukua kikombe kutoka kwa nabii TB Joshua, na kukipeleka mbele ya enzi ya Mungu.

Alisema Bwana alikuwa na malaika hawa akamchukua mchungaji mahala panapofaa kwasababualikuwa amemaliza mwendo wake duniani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents