Michezo

Novak Djokovic amtaka Andy Murray kujiandaa kisaikolojia kabla kushuka kwenye viwanja vya Queen Club

Mchezaji tennis raia wa Serbia, Novak Djokovic amemtaka Andy Murray kujiandaa kisaikolojia kwenye michuano hii ya Fever-Tree Championships ikiwa anarejea viwanjani kwa mara ya kwanza baada ya kuuguza majeraha yake kwa muda mrefu.

Murray haja cheza mechi za mashindano tangu apoteze hatua ya robo fainali ya michuano ya Wimbledon dhidi ya Sam Querrey na mchezaji huyo aliyekuwa nafasi ya kwanza kwenye viwango vya ubora duniani kupata majeraha yaliyompelekea kuwa nje ya uwanja tangu mwaka jana 2017 baada ya kufanyiwa upasuaji Januari.

Andy Murray athibitisha kushiriki michuano ya Fever-Tree Championships
Bingwa huyo mara tatu wa Grand Slam anatarajia kurejea uwanjani siku ya Jumanne kucheza na Nick Kyrgios mchezo wa raundi ya kwanza kwenye dimba la kwenye viwanja vya Queen Club huko West Kensington, London huku Djokovic akimuonya mchezaji huyo lazima ajiandae kisaikolojia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents