Michezo
Okrah kurejea Bechem United

BECHEM United ya Ghana imepanga kumrejesha nyumbani winga wa Yanga, Augustine Okrah aliyeonekana kutokuwa katika mipango ya kocha Miguel Gamondi. Imeripotiwa Waghana wamefungua milango kwa winga huyo aliyefanya vizuri akiwa na timu hiyo kabla ya kurejea Tanzania wakati wa dirisha dogo, awali aliichezea Simba.
