Michezo
Oscar Oscar: Msemaji wa Yanga Bumbuli anaongea kauli za hovyo kuwa wameshamaliza na Simba kivipi ? (+ Video)
Mtangazaji wa Efm na TVE Oscar Oscar ameeleza kuwa Yanga wanaweza kushinda kesi ya Morrison kwa sababu wapo na watu sahihi na wapo serious na kesi ile maana wamejiridhisha.
Mbali na hilo ameeleza kuwa endapo Yanga wasipopelekea timu uwanjani kama maneno yanavyosikika watakuwa wameleta picha mbaya sana na anaomba TFF wachukue sheria kufuata sheria za mpira ambapo timu inatakiwa kushuhwa madaraja mawili. pia amemtahadharisha msemaji wa Yanga Hassan Bumbuli kwa kauli zake anazozitoa kuwa Yanga ameshacheza na Simba wao wamebakiza michezo minne tu.