CEO wa Penthauze Music na mshindi wa tuzo mbalimbali za muziki, Phyno ambaye pia ni mtayarishaji wa muziki ameachia ngoma yake mpya iitwayo Full Current (That’s My Baby). Akishirikiana na mkali mwingine kutoka Nigeria Tekno.
Ngoma hiyo ya Phyno ‘Full Current’, inataja sifa za kipekee za mpenziwe ambapo ametumia mahadhi ya midundo ya Amapiano.
Kwa sasa ngoma hiyo inapatikana katika platform mbalimbali na pia ipo YOUTUBE. Mwaka 2021 rapa huyo kutoka Nigeria aliachia albamu yake ya nne iitwayo SOMETHING TO LIVE FOR ambayo bado inafanya poa huku akitarajia kuachia mawe mengine mampya siku zijazo.