Burudani

Picha: Diamond aitambulisha rasmi label ya WCB pamoja na ‘kumsainisha’ Rich Mavoko

Diamond Platnumz Ijumaa hii ameitambulisha rasmi label yake ya ‘WCB’ pamoja na kumsaini Rich Mavoko mbele ya waandishi wa habari.
Rich Mavoko akisaini mbele ya
Rich Mavoko akisaini mbele ya Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa, Godfrey Mngereza

Aidha, Diamond alimtambulisha dada yake, Queen Darleen kuwa mmoja kati ya wasanii wapya wa label hiyo.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa, Godfrey Mngereza ambaye alizungumza na kumpongeza Diamond huku akiwataka wasanii wengine kushirikiana kwa namna hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari katika hoteli ya Regency Park jijini Dar es salaam, Diamond amesema WCB imemsani Rich Mavoko ili kuleta chachu katika muziki.

“Nia ya kuwaita hapa ni kuonyesha kwamba wasanii tunaweza kushirikiana, tunaweza kufanya kitu kikubwa, ni muda wa kuonyesha sio ulimwengu wa vita kwa wasanii, watu wachukiane,” alisema Diamond. “Tukishirikiana wasanii kwa wasanii tutaonyesha mfano bora kwa jamii na hata mafanikio yataongezeka, kwa hiyo tuna Richard hapa na tunamshukuru sana, karibu kwenye familia,” alisema Diamond.

Kwa upande wa Rich Mavoko ameshukuru kusainiwa na WCB, huku akiwaahidi mashabiki wake mambo mazuri

“Mimi nizishukuru media zote ambazo zimefika kwenye shughuli hii maalum. Mimi nafikiri leo ni siku kubwa sana kwangu, kwa WCB pamoja na kwa tasnia ya muziki kwa ujumla. Lengo letu kubwa ni kuonyesha kwamba muziki wetu umefikia kwenye biashara kubwa sana, sisi tukionyesha umoja hata serikali itaweza kutusupport. Kwa hiyo sisi wasanii wenyewe kwa wenyewe tunabidi tuonyeshe undugu, pia serikali itaona sisi tupo serious kwenye kazi, kwa hiyo lengo la kuwa na Nasib WCB ni kufanya naye kazi, na nahaidi kufanya kazi nzuri zaidi ili kufikisha muziki wetu sehemu fulani,” alisema Rich Mavoko.

Pia Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza ambaye alihudhuria shughuli hiyo, alimpongeza Diamond huku akiwataka na wasanii wengine kushirikiana ili kuleta chachu kwenye muziki.

“Ni vizuri sana tunapo waona wasanii watanzania wanawekeza katika industry ya muziki, kwa hatua hii inaondoa ile dhana kwamba wanaoweza kuwekeza kwenye muziki ni watu toka nje, kwa hiyo ni hatua kubwa sana, ni hatua ya msingi sana ambayo Diamond na team yake yote wameipiga katika kuonyesha dhahiri kwamba kila kitu kinawezekana,” alisema Mngereza

Mavoko ambaye pia amechia wimbo uitwao ‘Story’, amesaini mkataba wa miaka 10.

Pia mmoja kati ya mameneja wa WCB, Sallam alisema mkataba huo haujamfunga Rick Mavoko kuondoka WCB, kama akihitaji kuondoka itabidi anunue mkataba huo ndipo aondeke.

Diamond na Mavoko wakibadilishana mikataba
Diamond na Mavoko wakibadilishana mkataba
Diamond na Mavoko wakipongezana
Diamond na Mavoko wakipongezana
Mavoko akisaini
Mavoko akisaini
Queen wa WCB
Queen wa WCB

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents