HabariSiasa

Polisi Zambia waizingira nyumba ya rais wa zamani Lungu, wanataka kuipekua

Polisi wa Zambia wameizingira nyumba ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Edgar Lungu katika mji mkuu, Lusaka, na kutaka kuipekua.

Wakili wa Bw Lungu, Jonas Zimba ameambia Diamond TV kwamba maafisa wa polisi wanafanya msako unaodaiwa kuhusishwa na umiliki wa magari matatu na hati miliki.

Alisema msako huo unafuatia malalamiko dhidi ya aliyekuwa mke wa rais, Esther Lungu, juu ya umiliki wake unaotiliwa shaka wa magari hayo matatu.

Polisi bado hawajatoa tamko kuhusiana na tukio hilo. Chama tawala cha zamani, Patriotic Front (PF), kimeelezea hatua hiyo kama ukiukaji wa kinga ya Bw Lungu kama inavyothibitishwa na sheria.

Bw Lungu aliondolewa mamlakani na Hakainde Hichilema katika uchaguzi wa Agosti 2021.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents