Baada ya Hospitali ya Muhimbili kuthibitisha kuwa wamefanikiwa kuwatenganisha mapacha walioungana, Leo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameandika kuwa:
“Nawapongeza Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kufanikisha upasuaji wa kuwatenganisha watoto mapacha walioungana. Hii ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mpango wa serikali kuboresha matibabu ya kibingwa. Nawaombea watoto Rehema na Neema wapone haraka”