Habari
Rais Samia awasili Songwe kuendelea na kampeni za uchaguzi mkuu

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Songwe kwa ajili ya muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho mkoani Songwe.
Kampeni hizo zinatarajiwa kuendelea mkoani Songwe leo Septemba 03, 2025 ambapo Rais Samia anatarajiwa kuzungumza na wakazi wa mkoa kwa kunadi sera za chama chake.

Written by Janeth Jovin







