Siasa
Rais Samia Suluhu arejea Dodoma akitoka Mwanza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma akitokea Jijini Mwanza baada ya kusimikwa kuwa Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani ni Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika leo tarehe 08 Septemba, 2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza.