Burudani
Rayvanny hakamatiki, awaimbisha mashabiki mwanzo mwisho (+video)
Msanii wa muziki kutoka WCB, Rayvanny usiku wa kuamkia jana alikuwa na show ya uzinduzi wa ziara ya Mr. Kiongozi jijini Tanga ambapo yeye alikuwa ndiye msanii pekee aliyetumbuiza kwenye jukwaa hilo.
Rayvanny alitumbuiza nyimbo zake zote huku akiimba mashabiki wake kila wimbo jambo ambalo liliibua shangwe za kutosha kwa mashabiki wake waliohudhuria show hiyo.