Kupitia kwenye kipindi cha RECAP & MANDO @el_mando_tz amezungumzia Tamasha la Wasafi Festival kwa baadhi ya show za wasanii ambao kwa upande wake anahisi wamefanya vizuri zaidi.
@el_mando_tz anasema kuanzia leo Rayvanny apewe jina la Mfalme wa Ubunifu Jukwaani kwa namna anavyobadilikabadilika kila show zake kwa ubunifu zaidi.
@el_mando_tz anasema kuwa Rayvanny ndio anapanikisha baadhi ya wasanii washindwe kufanya vizuri kwenye show zao wakihofia kufunikwa na Rayvanny.
Lakini pia kuna baadhi ya show za wasanii zimekuwa sio za kuvutia sana kutokana na kwamba wanazidisha zaidi manjonjo jukwaaani na kushindwa kutoa burudani vizuri kwa mashabiki.
@el_mando_tz amewapongeza wasanii wote akiwemo Mbosso, Ben Pol, Darassa, Zuchu, Billnass, Whozu na wengine ambao walifanya show nzuri kwenye Tamasha hilo.