RECAP: Bongo Fleva imeshuka Wasanii wanawekeza kwenye branding sio quality – El Mando

Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz amesema kadri silu zinavyoenda kuna namna muziki wetu umeanza kukosa ushindani hasa nje ya mipaka ya Tanzania.
Ukianzia Afrika Mashariki, Kenya, Uganda na mataifa mengine hata Rwanda kuna baadhi ya wasanii wapo serious sana na muziki hasa upande wa Ubora.
Ukija Tanzania kwa sasa Wasanii wetu damu changa wamewekeza kwenyw Kiki na Branding ila Ubora wa muziki umeanza kushuka kwa kasi kubwa.
Wasanii wakubali kukosolewa ili wajue wapi wanakosea na wapi warekebishe iki kuusongesha muziki wa Bongo Fleva.
Ukiangalia wasanii kama Kenya kwa sasa wanakuja kwa kasi sana kwa sababu wamejua Wasanii wa Tanzania wamekosea wapi.
Wanajua kabisa Tanzania Quality ya muziki ndogo sana ila wanapewa Airtime kubwa sasa wao wamewekeza kwenye ubora wa muziki.
Anasema baada ya miaka kadhaa Muziki wa Kenya utaupita muziki wa Tanzania.
Uchambuzi mzima upo katika akaunti yetu ya YouTube ya Bongofive.